Jumamosi, 15 Aprili 2017

Habari mbaya kwa wawekezaji waliopo na wanaotarajia kumiliki mabas... Jana tumeshuhudia kuwekwa kwa jiwe la msingi kufungua ujenzi wa train za umeme kutoka Dar mpaka Moro mradi utakao chukua muda wa miezi 30 sawa na miaka 2.5... Train hizo zinaweza kukupeleka Dar to Moro kwa saa 1:30 wakati mabasi yanachukua masaa 3:30 mpaka masaa 4:00 tofati n zaidi ya masaa 2:00... Train hizo zitakapo kamilika zinaweza kukimba kwa speed ya 160km/h wakati speed limit nyingi za barabarani ni 60km/h hichi n nini km sio kifo cha usafiri wa mabasi... Tujiulize je abiria wa kipindi hicho watachagua basi lenye kupigwa tochi, ulanguzi wa tiketi, ubovu,.. n.k au train za umeme zitazokua na uhakika wa safari tena bila kuchimba dawa wa kusimama kula? Na mm navyowafahamu wabongo kuna wakati pesa sio kitu mtu anaweza kulipa Tsh 650 akapanda Mwendokasi toka Kimara mpaka Ubungo ili awahi kuliko kupanda Eicher, Tata, n.k.. kwa gharama ya Tsh 400.. hvyo mradi wa train za umeme ukikamilika usishangae watu wakahama mabasi kwa wingi na wengine kuamua kuishi Moro kabisa kisa urahisi wa usafiri... Inavyosemekana miradi kama hii itaenda ruti za DAR-MORO-MZA, DAR-TANGA-MOSHI-ARS, na DAR-MORO-IRG-MBEYA kwa kufufua na kuboresha miundombinu tuliyoipotezea... Hii itaua kabisa biashara ya mabasi na malori pale itakapokamilika... Je wakati huo tutapost nn humu kama sio mabehewa na vichwa vyake na group kuitwa TANZANIA REGIONAL TRAINS...ambazo ni major ruti hapa nyumbani Tanzania... hii ni kwa nia njema tu na ss tuwe na maendeleo kama waliotutangulia... Kwa taarifa hii n vyema wawekezaji kuangalia watakua na nafas gani muda huo utakapofika... Shikamoo train za umemee

Kwa usafiri wa Mbeya_mwanza ngasamo express, premiere line na supershem express yapo kwa ajili ya wewe abiria

Alhamisi, 16 Februari 2017

Tilisho safaris

#TILISHO_SAFARIS;-
DAR _MARANGU_MWIKA_ROMBO_TARAKEA
TARAKEA_ROMBO_MWIKA_MARANGU_DAR.
#Kila_siku.
#NAULI=28000/=
   SEATS - 2×2 Full discount for all passengers.
#SEMI_LUXURY_DARAJA_LA_KATI.

Ijumaa, 10 Februari 2017

Flashback;scandinavia express

SOMA HISTORIA FUPI YA KAMPUNI YA MABASI YA SCANDINAVIA.

Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND  na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora  wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.
BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982

Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.

Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.

Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZILI.

KWA HISTORIA HII FUPI YA KAMPUNI YA SCANDINAVIA WAMILIKI WA MABASI WANATAKIWA AJIFUNZE KUWA NA HUDUMA BORA NA ZA VIWANGO VYA HALI YA KUMFANYA ABIRIA ASINUNG'UNIKE .
KUTOKA MAKTABA
SCANDINAVIA EXPRESS
PRINCESS CLASS
IN GOD WE TRUST

SCANIA F94 HB 310 HP
BODY BY CHODA FABRICATORS (K)  LTD
DAR-TUNDUMA BORDER

NISSAN DIESEL (UD)
BODY BY BANBROS (K)  LTD
DAR-KILIMANJARO-ARUSHA-NAIROBI-KAMPALA
#form_is_temporary_class_is_permanent

Tanzania buses specifications_part one(zhotong climber)

Technical Parameter

Dimensions
(mm)12500*2550*3850/3710G.V.W.(kg)21,500Max.Speed(km/h)120Approach Angle/Departure Angle(°)13º/10ºWheelbase(mm)5800+1350SeatsAdjustable type cloth seats ZTZY3210 2+2 layout 61+1 seats, (Fixing type cloth seatsZTZY3072,3+2 layout 70+1) , Driver seat ZTZY1050,Luggage Capacity(m3)10.4Fuel Tank (l)400L+400LEngine ModelL360 20Engine Output (kw/rpm)264Engine Max. Torque (N.m/rpm)1480Chassis ClutchCoil spring, Ø430Chassis Suspension SystemMulti-Leaf spring SuspensionChassis GearboxS6-160 ,ZF Technology, six gears, mechanismChassis Braking SystemDual circuit air braking, drum brakeChassis Steering SystemIntegral assistant power steeringFront Axle7.5 Ton front axleRear Axle13 Ton rear axleEnergy Storage System/Battery2×12V/195Ah / 28V /150A+140ATyre315/80R22.5Other FacilitiesBrake slack auto adjuster, Electric Retarder, ABSLength12m-13mSeats50seats+ModelIntercityEnergyDiesel

Tanzanian roads:part two

TUNAENDELEA NA IJUE TANZANIA NA MIKOA YAKE PAMOJA NA UMBALI WAKE;
SEHEMU YA 2.

RUTI YA MBEYA HADI DODOMA VIA MTERA.

RUTI YA MBEYA DODOMA KUPITIA MTERA  KM 601.

MBEYA - MAKAMBAKO (174KM)
Mbeya
Itewe
Inyala
Pipe line
Igulusi
Chimala
Igawa
Halali
Wanging'ombe
Makambako

MAKAMBAKO - MAFINGA (84km)  
Chimba dawa
Njiapanda ya mgololo
Kinegembasi
Maguani
Nyanyembe
Mbalamaziwa
Idetero
NYOLOLO
Vodacom
Misitu
Changarawe 
Mafinga

MAFINGA - IRINGA (80km)
Mafinga stand
Kinyanambo
Lungemba
Ulete
Ifunda
Ihemi
Njiapanda ya Mgama
Tanangozi
Mzani
Njiapanda ya Mlolo
Tosamaganga
Kitwuru
Bin mohamed
Ipogolo
IRINGA.

IRINGA - MTERA (BWAWANI) (123km)
Kihesa
mgongo
kilimahewa
mapana
Igingilanyi
kising'a
mkungugu
ndolela
isimani
kihorogota
Nyang'oro (kwenye mlima wenye kona kona kali na mabonde marefu)
kibaoni
izazi
MIGORI (HOTELINI)
Mkatapola
Mtera (bwawani panapozalishwa umeme wa gridi ya taifa)

MTERA - DODOMA (140km)

Kisima
Chipogoro
Seluka
fufu
manzase
mloda
mlowa
mpunguzi
mkonze
magorofani
DODOMA MJINI.

Source: Tanzania Regional Buses.

Tanzania regional roads:part two

T2 au Trunk road 2 ni barabara kuu ya Tanzania inayoanzia Chalinze mkoa wa Pwani kupitia Segera, Korogwe , Same, Moshi na Arusha  hadi mpaka wa Namanga. Huko  inaendelea mpaka Nairobi kwa jina la A104. Barabara hii ina urefu wa takribani kilomita 650 kwa upande wa Tanzania.
Kwa upande wa mabasi barabara hii inafanikisha ruti nyingi ikiwa pamoja na zile maarufu za Dar - Moshi - Arusha, Dar - Nairobi, Dar - Karatu, Dar - Rombo na Dar - Tanga. Inatumika na mabasi zaidi ya 100 ya kampuni zaidi ya 40 kila siku.
T2 ndio barabara ya kwanza Tanzania kuwa na mabasi aina ya Marcopolo yaliyoletwa na kampuni ya Royal coach kwa ruti ya Dar - Moshi - Arusha. Na ndio barabara yenye mabasi mengi aina ya Marcopolo kwa sasa.
T2 pia ndio barabara ambayo ambayo ina hoteli nzuri zaidi na migahawa inayohudumia abiria kwa njia ya mabasi,malori na magari binafsi (huduma, vyakula vizuri na vinywaji)
Ukitumia barabara ya T2 utaweza kuona daraja maarufu la Wami, Mlima mrefu zaidi Africa (Kilimanjaro), Mlima Meru na  Milima ya Upare bila kusahau huduma ya mananasi na machungwa ya kutosha pale Chalinze, Segera na Korogwe.